SEHEMU YA NNE
SIMULIZI: HATIA TAKATIFU
Mwandishi: Kedmund Mtembezi
Email kedmund742@gmail.com
WhatsApp+255 672 229 424
SEHEMU YA 4
Gari lilikuwa linatembea kwa kasi usiku wa manane. Taa za barabarani zilikuwa zinapita kama mistari ya mwanga kwenye macho ya Kedmund.
Hakuna aliyekuwa anaongea.
Moyo wake ulikuwa unapiga kwa nguvu, lakini safari hii haikuwa hofu ya polisi… ilikuwa hofu ya kitu kisichojulikana.
Walifika kwenye jengo moja la kifahari zaidi kuliko lile la Rashid. Hapa kulikuwa na ulinzi mkali — walinzi, kamera, kila kitu kilionyesha hii ni level nyingine.
“Mshuke,” mmoja wa wale wanaume alisema.
Kedmund alishuka taratibu, macho yake yakizunguka kila kona.
Alipelekwa ndani… hadi kwenye chumba kikubwa kilichokuwa na taa za rangi laini.
Ndipo alipomwona.
Alikuwa amekaa kwenye sofa, akivuta pumzi polepole kama mtu asiye na wasiwasi wowote duniani.
Msichana.
Mzuri kuliko yeyote ambaye Kedmund alikuwa amewahi kuona.
Ngozi yake iling’aa chini ya mwanga, macho yake yalikuwa makali lakini yenye mvuto, na tabasamu lake lilikuwa la hatari.
“Karibu,” alisema kwa sauti laini.
Kedmund alisimama kimya kwa sekunde chache.
“Mimi naitwa Amina.”
Jina hilo lilikaa kichwani mwake.
“Kedmund,” alijibu kwa tabu kidogo.
Amina alisimama, akamkaribia taratibu. Alikuwa anatembea kwa kujiamini kama mtu anayejua nguvu yake.
“Nilikuwa nasikia habari zako…” alisema huku akimzunguka kama anamsoma.
“Unaanza vizuri kwenye mchezo.”
Kedmund alishangaa.
“Wewe ni nani hapa?” aliuliza.
Amina alitabasamu kidogo.
“Mimi ni sehemu ya mchezo huu… lakini siyo mtu mdogo kama unavyofikiria.”
Kabla hajaendelea kusema, mlango ulifunguliwa.
Rashid akaingia.
Safari hii, hakuwa peke yake. Alikuwa na mwanaume mwingine mwenye sura kali zaidi — macho yake yalikuwa baridi kama barafu.
“Huyu,” Rashid alisema, “ndiye mtu mkubwa hapa. Tunamwita Mzee.”
Kedmund alihisi presha ikipanda.
Mzee alimwangalia kwa makini.
“Wewe ndiye kijana mpya?” aliuliza kwa sauti nzito.
“Ndiyo,” Kedmund alijibu.
Mzee alikaa chini polepole.
“Ninapenda vijana wenye njaa ya maisha… lakini sipendi wasaliti.”
Chumba kilinyamaza.
Kedmund alihisi uzito wa maneno hayo.
Baada ya mazungumzo mafupi, Kedmund aliruhusiwa kuondoka.
Lakini kabla hajaenda, Amina alimfuata nje.
“Subiri,” alimwita.
Kedmund alisimama.
Amina alimsogelea karibu sana… karibu kiasi kwamba aliweza kuhisi pumzi yake.
“Usiwaamini sana hawa watu,” alisema kwa sauti ya chini.
Kedmund alishangaa.
“Kwanini?”
Amina alimtazama moja kwa moja machoni.
“Kwa sababu kila mtu hapa anacheza mchezo wake mwenyewe.”
Maneno hayo yalimchanganya.
Lakini kabla hajauliza zaidi, Amina alitabasamu tena kama hakuna kilichotokea.
“Tutaonana tena,” alisema, kisha akaondoka.
Siku zilizofuata, Kedmund alijikuta akimfikiria Amina mara kwa mara.
Si tu kwa uzuri wake…
Bali kwa maneno yake.
Kulikuwa na kitu ndani yake kilichovutia — lakini pia kilitisha.
Siku moja usiku, simu yake iliita.
Namba mpya.
Alipokea.
“Sauti hii utaikumbuka?” ilikuwa ni Amina.
Moyo wake uliruka kidogo.
“Amina?”
Alitabasamu upande wa pili.
“Good… hujasahau.”
Waliongea kwa muda mrefu usiku huo.
Mazungumzo ya kawaida yakageuka kuwa ya karibu zaidi.
Kedmund alihisi kitu kipya — kitu ambacho hakikuhusiana na pesa wala hatari.
Alianza kumpenda.
Lakini…
Hakujua kuwa Amina alikuwa na siri kubwa.
Usiku mwingine, mbali na macho ya kila mtu, Amina alikutana na mtu kwenye gari.
Mwanaume aliyekuwa tofauti kabisa na wale wa Rashid.
“Huyo kijana anaingia sana kwenye mfumo,” mwanaume alisema.
Amina alinyamaza kwa sekunde chache.
“Kazi yangu ni kumuweka karibu… siyo kumuonea huruma,” alijibu.
Mwanaume alitabasamu kidogo.
“Usisahau lengo letu.”
Amina aliangalia mbali… macho yake yakionyesha mgongano wa hisia.
Wakati huo huo, Kedmund alikuwa anaingia ndani zaidi ya penzi hilo.
Hakujua kuwa kila tabasamu la Amina…
Kila simu…
Kila neno la karibu…
Likuwa linaweza kuwa sehemu ya mchezo mkubwa zaidi.
Mchezo wa usaliti.
Usiku mmoja, walikutana.
Walikaa pamoja, wakiongea, wakicheka.
Kedmund alimshika mkono Amina.
“Kuna kitu nakuhisi… siwezi kuelezea,” alisema kwa ukweli.
Amina alimtazama kwa muda mrefu.
Kwa mara ya kwanza…
Tabasamu lake lilionekana la kweli.
Lakini ndani yake, kulikuwa na vita.
Kwa sababu alijua ukweli mmoja:
👉 Moyo wake unaanza kuingia… lakini kazi yake ni kumuangamiza Kedmund.
Mwisho wa Sehemu ya 4
#Like_comment Tuendelee sehemu ya 5.
Maoni
Chapisha Maoni